KUISHI MAISHA YA USHINDIImekuwa ni matatanio ya kila mwanadamu kuishi maisha
ya ushindi lakini hayo matamanio hutofautiana baina ya mtu mmoja na mwingine
hii ni kwa sababu ya mitazamo kutofautiana.Ukisoma katika biblia utaona utaona jinzi Mungu
alivyo mkusudia binadamu aishi maisha ya ushindi ndio mana ukiangalia uumbaji
wa binadam ni tofauti na uumbaji wa vitu vingine MWANZO 1:6-24 Mungu alipoumba
vitu vyote alitamka kiwepo hiki na kikawepo lakini ulipokuja uumbaji wa binadam
ulikua katika majadiliano kati ya MUNGU BABA, MUNGU MWANA NA ROHO
MTAKATIFU{TRINITY} Mwanzo 1:26 biblia inasema na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu wakatawale…………kwa hiyo
tunaona dhahiri kwamba Mungu alishirikisha cabinet lake mbinguni katika
kumuumba binadam na huyo binadamu aliubwa atawale.Pia uumbaji wa binadam ulikuwa katika process Mwanzo2:7&18&21-22
uumbaji wa binadam ulikuwa katika hatua biblia inatuambia yalichukuliwa mavumbi
ya ardhi ambayo yaliumba mtu asie hai, ili mtu awe hai Mungu alimpulizia pumzi
yake hatmaye akawa nafsi hai vile vile uumbaji wa HAWA.Kabla
sijaendelea na kujikita katika somo ningependa tujiulize ni upi mfano wa mungu
kumbuka hatujaubwa kama Mungu lakini tumeubwa kwa mfano wake.Biblia inamuelezea kuwa Mungu ni ROHO Yohana 4:23 Mungu ni Roho nao wamwabuduo imewapasa
kumwabudu katika Roho na kweli. Kwahiyo binadamu kuna namna ambayo aweza
akaishi kama Roho(kuishi Rohoni).
No comments:
Post a Comment